Tunawatakia Heri ya Mwaka Mpya
Posted on December 31, 2025, 11:02 pmHappy birthday Mwalimu Goodluck Mjule
Posted on December 27, 2025, 1:52 pm
Happy birthday Mwalimu Rashid idd msuya
Posted on December 27, 2025, 1:51 pm
Habari Wazazi/Walezi, Shule ya Msingi Mwanzugi inapenda kukutakia kheri ya siku ya krismas wewe na wapendwa wako. Ahsante kwa kuwa pamoja nasi
Posted on December 25, 2025, 9:56 am
18/12/2025
Posted on December 18, 2025, 8:23 am
Shule imefungw Tarehe 05/12/2025 na itafunguliwa Tarehe 13/01/2026,
hivyo kila mzazi/mlezi hakikisha kipindi cha likizo unafanya mambo yafuatayo kwa mwanao
1.Kumuandalia vifaa vyote vya kujifunzia mfano madaftari,sare za shule ,karamu na vinginevyo
2.Kumfuatilia maendeleo yake baada ya kupokea taarifa ya matokeo na maendeleo yake shuleni
3.Kumlinda na kumuhimiza umuhimu wa shule pia kumtahadharisha na mambo mabaya ya kijamii haswa kipindi hiki cha likizo
4.Siku ya kufungua shule afike kwa wakati ili aweze kuendelea na masomo
Hivyo shule ya msingi mwanzugi inawatakia wanafunzi wote likizo njema na heli ya Krismass na Mwaka mpya
KWA MAWASILIANO ZAIDI TUPIGIE KWA NAMBA ZIFUATAZO
1.MWALIMU MKUU 0753576431
2.MWALIMU MKUU MSAIDIZI 0621295401
3.MTAALUMA WA SHULE 0627555552
Posted on December 9, 2025, 7:23 pm
Mwalimu mkuu Saidi Hayawi Leo Tarehe 04/12/2025 ameteua kamati mbalimbali za shule.
Kamati hizo zitaanza kazi mara moja kwa ajili ya mwaka 2026
Posted on December 4, 2025, 3:55 pm
Muandikishe mwanao sasa
Posted on November 29, 2025, 9:14 am
Afisa Elinu Mkoa wa.Tabora,Mwl Upendo Rweyemamu ametoa rai kwa wazazi na walezi kuhakikisha wanaandikisha watoto wao kwa ajll ya elimu
ya awali na darasa la kwanza mapema kwa ajli ya mwaka wa masomo
2026,ili kutoa nafasi kwa Serikali na wadau wa elimu kufanya maandaliziya
miundombinu na rasilimali muhimu kwa wakati.
Amesema hatua ya uandikishaji wa mapema husaidia kupanga vyema idadi
ya madarasa,walimu na vifaa vya kujifunzia,hivyo kuboresha mazingira ya
ujfunzaji na kuhakikisha kila mtoto anapata haki yake ya msingi ya elimu.
Wakati huohuo,Mwl.Rweyemamu amesisitiza umuhimu wa jamil
kutowaacha nyuma watoto wenye mahitaji maalum,akibainisha kuwa
Serikali imeendelea kuimarisha miundombinu rafiki na kuanzisha shule
maalum na madarasa shirikishi kwa ajlli ya kuwatambua,kuwawezesha na
kuwapatia huduma stahiki za elimu bila ubaguzi.
βLakini pia tuna watoto wenye mahitaji maalum ambao wapo kwenye
nyumba zetu,tusiwasahau tumejiandaa kuwapokea,kama unaye mtoto
mwenye mahitaji maalum hakikisha naye pia anaandikishwa,"amesisitiza.
Posted on November 27, 2025, 7:59 pm
Tarehe 21/11/2025 mwalimu mkuu amefanya kikao Cha wazazi wa darasa la sita na kueleza mikakati mbalimbali ya kuinua Taaluma na kukuza ufaulu kwa darasa la sita
Katika kikao hicho mwalimu mkuu ameongelea mambo mbalimbali kama ifuayavyo
1.Kuwajali wanafunzi kwa kuwanunulia vifaa vya kujifunzia na sare za shule
2.Kuwafaatilia watoto wao maendeleo ya shule kwa kutumia mfumo wa matokeo unaoitwa mwanzugi.com
3.Kuwa karibu baina ya mzazi na Walimu ili kumuendeleza mwanafunzi
Pia wazazi wamekubaliana kuwa wanafunzi wa Darasa la sita wasifunge shule na wasome kwa wiki tatu wakati wa likizo
Pia Kuwanunulia wanafunzi vifaa vifuatavyo
1.counter book query 3 saba
2.Daftari za msomi saba kwa ajili ya majaribio
3.Kuchangia kiasi cha Tsh. 5,000/= kwa ajili ya mitihani na motisha kwa walimu watakaokuwa wanafundisha wakati wa likizo
Pia mwalimu mkuu amewaomba wazazi kuisemea vizuri shule ya Msingi mwanzugi ili iweze kutangazika vyema
Posted on November 22, 2025, 8:36 pm